15 December 2010

WAKIMBIZI 27 WAUAWA NA AJALI MBAYA AUSTRALIA

Boat inayosadikiwa kubeba watu wanaodaiwa kuwa wakimbizi(Asylum seeckers) imegonga mwamba pembezoni mwa ufukwe wa kisiwa cha Christmas nchini Australia.Watu hao ambao wanahisiwa kutokea nchi za Iran na Iraq walikumbwa na mkasa huo baada ya Injini ya boat hiyo kushindwa kufanya kazi,tatizo ambalo liliifanya hitimisho la safari yao kushambuliwa na hali mbaya ya hewa iliyozua mawimbi yaliyo isukuma boat hiyo kwenye ukingo wa mawe(Rock cliff).Mpaka sasa watu 27 wanasadikiwa kupoteza maisha.na 42 wameokolewa.

Angalia window hapo chini bofya SEE MORE VIDEO kwa habari hii na nyingine toka Australia leo:




Tatizo la wakimbizi kutumia njia ya boat kuingia Australia kupitia kisiwa hiki imekuwa kubwa kwa serikali na hasa katika kambi ya wakimbizi ya kisiwa hicho cha Christmas ambacho kina kabiliwa na mfuriko wa wakimbizi kwenye kambi hiyo.
--the Austrian

More links:
http://www.foxnews.com/world/2010/12/14/asylum-seeker-boat-capsizes-australia/?test=latestnews
http://www.bbc.co.uk/news/world-asia-pacific-11997231

No comments: